Baada ya serikali kusitisha agizo la Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) lililokataza TV za mitandaoni zisiendelee kutoa huduma, Michuzi TV imerudi hewani kwa kishindo huku ikiwaahidi wadau wote kwamba mambo sasa yatakuwa motomoto kuliko ilivyokuwa awali. 
Serikali imesitisha agizo hilo la TCRA baada ya kuonekana halina mantiki kwa vile kanuni za namna ya kuendesha huduma hii hazipo tayari na kuzuia ni kutowatendea haki wananchi wanaofurahia huduma hii bila malipo. Michuzi TV itaendelea kupiga mzigo huku ikisubiri na hatimaye kutii kanuni zozote zitazowekwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...