Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World Customs Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya akisisitiza jambo wakati wa kikao cha pamoja na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia) alipotembelea TRA ili kujadili masuala mbalimbali na kuona maendeleo ya miradi ya Forodha inayotekelezwa na TRA kwa ushirikiano na WCO
Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World Customs Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya (kulia) akifurahia zawadi ya kitabu cha historia ya Tanzania ambacho Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata alimkabidhi kama ishara ya ukumbusho wa ziara yake nchini Tanzania. Dk. Mikuriya alitembelea TRA ili kujadili masuala mbalimbali na kuona maendeleo ya miradi ya Forodha inayotekelezwa na TRA kwa ushirikiano na WCO.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Alphayo Kidata (kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World Customs Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya alipotembelea TRA ili kujadili masuala mbalimbali na kuona maendeleo ya miradi ya Forodha inayotekelezwa na TRA kwa ushirikiano na WCO
Meneja Mifumo ya Kielektroniki ya  Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Bw. Tinkasimile Felix (aliyesimama) akitoa maelezo ya jinsi Mfumo wa Forodha (TANCIS) unavyofanya kazi kwa Katibu Mkuu wa Shirika la Forodha Duniani (World Customs Organisation-WCO) Dk. Kunio Mikuriya (aliyeketi katikati). Wengine ni Meneja wa Maendeleo Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini kutoka Shirika la Forodha Duniani Bw. Patrick Gyan (kushoto) pamoja na Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa Bw. Jocktan Kyamuhanga (kulia).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...