Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi
wa habari kuhusu maandalizi ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa
kufanyika wakati wa sikukuu ya Pasaka jijini Dar es salaam, Msama
amesema maadalizi yanaendelea vizuri na wako kwenye mazungumo na
waimbaji kutoka mataifa mbalimbali kama vile Rwanda, Nigeria, Afrika
Kusini Zambia na kwingineko ili kuboresha Tamasha hilo ambalo pia
litafanyika katika mikoa kumi ya Tanzania.
Ameongeza
kwamba Tamasha la mwaka huu pia lina kazi kubwa ya kumuombea Rais Wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk.John Pombe Magufuli kwa kazi
kubwa anayoifanya kuleta Maendeleo kwa watanzania lakini pia kupambana
na vita mbaya ya Madawa ya Kulevya.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua jambo kwa
waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Tamashahilo wakati
alipozungumza na jijini Dar es salaam jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...