Na Haji Manara


Baada ya ushindi Musharraf wa hapo jana dhidi ya Majimaji wa goli tatu kwa bila, naamua kuperuzi mitandaoni kujua nn kimejiri huko, nn kimeandikwa na makocha wetu mahiri wa kukosoa, nakutana na vibweka vilevile vya siku zote, ahhh naamua kutoka huko na kuongea na wanangu masuala yao ya shule!!

Nimeanza na aya hiyo nikimaanisha kitu, tena kitu chenyew kwa sasa kishakuwa kama 'URADI'au ada, ni ukosoaji wa viwango vya majitaka, hususan pale Simba inapofungwa, na bad luck ukosoaji huo wa ajabu hufanywa na baadhi ya mashabiki wetu,

Mechi yetu ya mwisho tulipogongwa na Azam, ilikuwa kama jenahannam kwa sisi viongozi wa simba, hasa huku mitandaoni, ukiachana na hoja zao za tulikuwa tunaongoza ligi kwa points nane na sasa tumezidiwa na Yanga kwa points moja, ipo hoja nyingine ya wakosoaji, wanadai tumekaa miaka minne bila kuchukua ubingwa!!

Nianze na hili la points nane, ikiwa tuliwapita wenzetu kwa tofauti hyo ya points, nini ajabu Simba kupitwa point moja? factor moja ambayo haizungumzwi na wakosoaji ni je hzo points tumepoteza na nani na wapi? na kwa nn tulipoteza hizo points, hebu msomaji isafirishe akili yako na ujipe majibu mwenyew!!

Hili la kutochukua ubingwa miaka minne, je uongozi huu una muda gani ktk miaka hyo minne? na je hii ni mara ya kwanza hili kutokea kwa Simba au Yanga?hv mnazo kumbukumbu sahihi vjana wa dotcom?

Kwangu mm naamini huu ni mwaka wetu, ni mwaka ambao uongozi wenu umeamua kwa maksudi kuwapa furaha wanasimba, na ndio maana mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Azam, kuna hatua mahsuus ulizochukua, ambazo sisi tunaamin ztatusaidia sana kupata tunalolihitaji.Wanaasimba mpira wa miguu haupo kwa ajili ya kushinda kila siku,haupo kwa ajili ya ww kufurahi siku zote,,ukitaka kuamini hilo, nakusihi sana,achana na mchezo huu,,ruksa kupenda mchezo mwingine, Ajabu yetu timu ikifungwa wabaya ni viongozi, ikishinda wanaosifiwa ni wachezaji,

uogozi ulaumiwe kama mahitaji ya wachezaji hayatimizwi, sasa tumefungwa na Azam, viongozi hawafai, tumeshinda na Majimaji, KIAMA Kimerudi, uhhh lalaaa!!
lau mngejua juhudi zilizochukuliwa na uongozi hadi timu kurudi mchezoni kule Songea, mngekuwa mnaweka akiba ya maneno, mngekuwa hamtoki povu bila sababu yoyote,
Na kwa hili Mungu amekuwa upande wetu, lau Game na Majimaji ingekuwa dar, tungefungwa au kudroo, washabiki wengi wa dar hujitia ujuaji wasiokuwa nao, kutwa kushinda mitandaoni kuponda, lakini angalia walichofanya Songea, uwanja umetapika kama hatujatoka kufungwa, njiani ni Simba tu, kwetu hili liwe funzo, mpira hauchezwi ktk magrup ya watsapp, hauchezwi fb au insta, unachezwa uwanjani, na kuna vtu vingi vnavyofanya timu ipate matokeo.
Leo wapo baadhi yetu wanajiona wao ndio Simba zaid kuliko wengine, wanadhan wao ndio huumia timu inapofungwa kuliko wenzao, sasa hawa tuwaangalie huko mitandaoni, hawa wana nia ya kutugawa, wana nia ovu, na tusiwapuuze, tuwaondoe kuwa miongoni mwetu.
Jambo la msingi kwa sasa ni kupata points tatu kwa kila mchezo unaokuja, tunahitaji umoja kuliko kipindi chochote kile,tunahitaji kushauriana sio kukashifiana au kutukanana, Simba watsapp tunawahitaji sana ila kwa lengo la kujenga sio kubomoa,Najua wengine wataona nawakashifu, hapana, nawaambia ukweli na wakiona mchungu, hiyari yao,
Mwisho niwaambie kocha mkuu wa Simba ni mmoja tu, hatuwezi kuchukua ubingwa kwa kuwa na makocha lukuli wa mitandaoni, tuwape benchi la ufundi nafasi.
Tamati yangu ni kuwaomba tena na tena, mitandao isitumike kupotosha na kuzua uongo, mitandao itumike kiufasaha kwa maendeleo yetu, sio kutusi watu kwa kuwa upo mbali nae, maana tunajua wengine hutafuta kiki mitandaoni,
Tusonge mbele na tuanze na  Prisons kisha Gongowazi aje.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...