Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo Zamaradi Kawawa akizungumza juu ya Bonanza hilo
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Theophil Makunga akizungumza na waandishi wa habari juu ya Tamasha hilo

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Waziri wa habari Sanaa, utamaduni na Michezo, Nape Nnauye anataraji kuongoza  Bonanza la mazoezi na upimaji afya February 18 mwaka huu ulionadaliwa na Chama cha maofisa mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa kushirikiana na jukwaa la wahariri Tanzania na Dar es Salaam City Press Club.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Msemaji wa chama TAGCO, Abel Ngapemba ametaja kuwa lengo la Bonanza hilo ni kuhamasisha wananchi kujenga tabia ya kufanya mazoezi na kupima afya kama ilivyozoeleka kwa kuunga mkono kampeni iliyozinduliwa na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan.

“washiriki wa bonanza hili ni pamoja na maofisa mawasiliano wa Serikali na wasekta binafsi ,Wahariri , Wahandishi wa habari na Bloggers na wananchi kwa ujumla kwa kuongozwa na Waziri Nape Nnauye na kuhudhuliwa na viongozi wa Wizara ya afya na ustawi wa jamii, jinsia wazee na watoto” amesema  Abel.

Ametaja kuwa mbali ya mazoezi taasisi zitakazo shiriki kutoa huduma siku hiyo ni pamoja na Tasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Hospitali ya Saratani ya Ocean Road,Hospitali ya Sanitas,CCP Medicine Kinyerezi na Mfuko w Bima ya Afya (NHIF), Chama cha madaktari wa meno Tanzaniana tasisi ya wagonjwa wa mifupa MOI.

Abel ametoa wito kwa wahariri wa vyombo vya habar, waandishi wa habari , Bloggersna maofisa mawasiliano Serikalini, mashirika binafsi na tasisi za kimataifa kujitokeza kwa wingi katika bonanza hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...