Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, tarehe 08 Februari, 2017 amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa jengo jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam (Terminal 3) na kuagiza shughuli za ujenzi wa uwanja huo ziendelee kuanzia kesho.
Awali Mkandarasi anayejenga uwanja huo ambaye ni kampuni ya BAM International alitangaza kusitisha ujenzi kuanzia leo kutokana na kutolipwa madai yake na Mhe. Rais Magufuli ameahidi kulipa fedha hizo haraka.
Hata hivyo, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa kwake na namna mradi huo unavyotekelezwa ikiwemo Serikali kukubali gharama kubwa za mradi ambazo ni Shilingi Bilioni 560 kiwango ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na jengo linalojengwa.
“Hivi kulikuwa na sababu gani za nyinyi wataalamu wa Serikali kukubali gharama kubwa namna hii, hivi hili jengo linafanana na Bilioni 560?
“Halafu mlikuwa na haraka gani kuidhinisha kuanza awamu ya pili ya ujenzi kabla ya kumaliza awamu ya kwanza?” amehoji Mhe. Rais Magufuli alipokuwa akiwauliza Wahandisi wa Wizara ya Ujenzi wanaosimamia ujenzi huo.
Kufuatia hali hiyo, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa Mnyaa aliyeongozana nae kuunda timu ya wataalamu watakaofanya tathimini ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuzungumza na Mkandarasi anayejenga uwanja huo na Mhandisi Mshauri ambao wamekubali kupunguza gharama za ujenzi wa mradi huo.
“Serikali italipa fedha ambazo Wakandarasi wanadai lakini, nataka Waziri uunde timu ya kufanya tathmini upya, ni lazima hii gharama ipungue, hatuwezi kumaliza fedha zote hizi wakati jengo halifanani na thamani hiyo” amesisitiza Dkt. Magufuli.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli ambaye ameonesha kutofurahishwa na dosari zilizoanza kujitokeza katika baadhi ya maeneo ya jengo hilo, amemuagiza Mhe. Waziri Mbarawa kuunda upya timu ya Wahandisi watakaosimamia mradi huo na ambao watafanya kazi kwa uzalendo na kusimamia ubora.
Kabla ya kuondoka uwanjani hapo Mhe. Rais Magufuli amekutana na wafanyakazi walioajiriwa katika shughuli za ujenzi wa uwanja huo na kuwahakikishia kuwa Serikali imechukua za kuhakikisha mradi huo unaendelea na kwamba kuanzia kesho wataendelea na kazi kama kawaida.
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemsimamisha kazi Kaimu Katibu wa Tume ya Mipango (Wizara ya Fedha) Bi. Frolence Mwanri aliyeidhinisha kuanza kwa awamu ya pili ya ujenzi wa jengo hilo jipya la Uwanja wa Ndege kabla ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ili kupisha uchunguzi.
Mhe. Dkt. Magufuli ameviagiza vyombo vinavyohusika kufanya uchunguzi katika mradi huo. 

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

08 Februari, 2017 


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa Terminal III kuona maendeleo ya ujenzi unaondelea leo Jumatano February 8, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa Terminal III kuona maendeleo ya ujenzi unaondelea leo Jumatano February 8, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa Terminal III kuona maendeleo ya ujenzi unaondelea leo Jumatano February 8, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa Terminal III kuona maendeleo ya ujenzi unaondelea leo Jumatano February 8, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  katika picha ya pamoja na baadhi ya wahandisi na makadrasai alipofanya ziara ya kustukiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa Terminal III kuona maendeleo ya ujenzi unaondelea leo Jumatano February 8, 2017.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...