Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za vifo vya mashabiki 17 na wengine kujeruhiwa katika tukio la watu kukimbia uwanjani kwa tishio la mabomu wakati wakati wa mchezo wa timu mbili zenye ushindani. 
Maelfu ya mashabiki, wakiwamo watoto wadogo walianza kukimbia na wengine kukanyagana hali iliyosababisha vifo uwanjani. 

Rais Jamal Malinzi wa TFF, ameelezea kushtuka kwa taarifa hizo za vifo hivyo vinavyoripotiwa kutokea Ijumaa Februari 10, 2017 kwenye Uwanja wa Angola ulioko mjini Uige, Kaskazini mwa nchi hiyo.  
Kwa masikitiko makubwa, Rais wa TFF Malinzi ametuma salamu zangu za rambirambi kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Angola (AFF); familia za ndugu waliopoteza wapendwa wao katika maisha, watu wa nchi hiyo, kutokana na vifo hivyo. 
Rais Malinzi amesema kwa nguvu za Mungu anawaombea heri ya kupona majeruhi na kwamba Tanzania inasali kuwaombea watu wa Angola wakati huu mguu. 
Mwenyezi Mungu azipokee roho za marehemu mahali pema peponi.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA 
MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...