Na Stella Kalinga 
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini ametoa wito kwa viongozi na Wakuu wa Taasisi za Umma mkoani humo,  kusimamia utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi ya viungo Jumamosi ya pili ya kila mwezi. 
Sagini ametoa wito huo leo katika hotuba yake kwa watumishi wa umma,wanafunzi na wananchi walioshiriki mazoezi ya viungo na michezo mbalimbali katika uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mhe.Makamu wa Rais. 
Amesema Simiyu wamejipanga kutekeleza na akawataka watumishi wa Umma kuheshimu agizo hilo na kutekeleza kama ilivyoelekezwa, badala ya kuamua kushiriki au kutoshiriki. 
"...Niombe wote wanaowasimamia Watumishi wa Umma kuhimiza utaratibu huu wa mazoezi ambao ni agizo la Makamu wa Rais ambalo limeongozana na nyaraka za Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara yenye dhamana na Elimu na Mafunzo ya Ufundi, lakini mara kadhaa hata Wizara ya Afya imekuwa ikisema,  Sisi kama Watumishi wa Umma hatuwezi kuchagua kutekeleza au tusitekeleze" alisema. 
Amesema kila mkuu wa Taasisi,Idara,Sehemu anapaswa kuhakikisha watumishi walio chini yake wanashiriki mazoezi ya viungo mwezi ujao(Machi) kwa kuwa  kushindwa kutekeleza Maelekezo ya viongozi pasipo sababu za msingi ni utovu wa nidhamu, ambalo ni kosa kwa mujibu wa Sheria,kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.
 Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini (mwenye kofia nyeupe) akiwa na baadhi ya watumishi  katika mazoezi ya kutembea kwenye Uwanja wa Halamshauri ya Mji Bariadi, wakati wa utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi ya Viungo.
 Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini (wa pili kushoto) akishiriki mazoezi ya viungo na  baadhi ya watumishi wa Umma,wanafunzi na wananchi katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.
 Timu ya Sekretarieti ya Mkoa ikivuta kamba dhidi ya timu ya Halmashauri ya Mji Bariadi (haipo pichani) katika  Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.
 Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akizungumza na Viongozi na watumishi wa Umma, wanafunzi na wananchi walioshiriki mazoezi ya viuongo na michezo mbalimbali mjeni Bariadi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan. 
 Baadhi ya watumishi wakishiriki mbio za mita 100 wakati wa utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi ya Viungo na michezo mbalimbali mjini Bariadi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...