Na Pamela Mollel,Arusha 
 Imeelezwa kuwa siku ya sheria ni siku ambayo wananchi wanapata fursa ya kupata msaada wa kisheria ambayo kila mwananchi anapaswa kuwa chini ya shieria na sio juu ya sheria. 
 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakili wa kujitegemea Mruma aShabibu kutoka kampuni IRM Legal alisema kuwa siku hii ni maalum kwa mawakili kutoa huduma za kisheria kwa jamii bila malipo yeyote. 
 Alisema kuwa kwa siku hii watu wengi ufaidika kwa kutatuliwa baadhi ya matatizo yao bila kutozwa gharama yeyote ikiwa ni pamoja na kupata elimu ya kisheria sanjari na kupata fursa ya kubadilishana mawazo na mawakili. 
 Alidai kuwa wananchi wanapaswa kuheshimu katiba lakini pia na kukaa chini ya sheria ili haki iweze kutendekea kwani baadhi ya wananchi wanakaa juu ya sheria hali ambayo inawafanya kujiona hawatendewi haki. 
 Hata hivyo alifafanua kuwa lengo la kuanzishwa kwa siku hii ni kuangalia umuhimu wa sheria katika jamii na kuona jinsi inavyofanya kazi katika kukuza uchumi wa nchi
Wakili wa kujitegemea Mhe. Mruma aShabibu kutoka kampuni  IRM Legal  anasema kuwa siku hii ni maalum kwa mawakili kutoa huduma za kisheria kwa jamii bila malipo yeyote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...