Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
mkoani Shinyanga, Stephen Magoiga ameagiza watendaji wa vijiji kuhakikisha
wananchi waliochukua fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Taifa (TASAF) bila kuwa na
sifa wanarudisha mara moja.
Magoiga alitoa agizo hilo jana wakati akifungua mafunzo
kwa wadau wa TASAF kwa vijiji vitatu katika Kata ya Mwakipoya ili kuwajengea
uelewa katika kuwaudumia walengwa.
Alisema lengo la mpango wa TASAF ni kusaidia kaya
zisizo na uwezo hivyo ni wajibu wa wadau hasa wajumbe wa Serikali za vijiji kuhakikisha
wanawatambua wananchi wa maeneo yao ili kubaini kaya maskini.
Mkurugenzi aliwataka wadau kusimamia vizuri walengwa akisisitiza
kuwa Serikali kupitia TASAF ina jukumu la kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na
maisha bora kwa kuwapa ruzuku ili kujiendeleza.
Magoiga aliongeza kwa kuwahimiza wadau hao kufuatilia
maendeleo ya watoto wa walengwa wa mpango huo wanaopata ruzuku kwani elimu
ndiyo inaweza kuondoa umaskini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Stephen Magoiga akifungua rasmi mafunzo kwa wadau wa TASAF kwa vijiji vitatu katika Kata ya Mwakipoya ili kuwajengea uelewa katika kuwaudumia walengwa.
Mratibu wa TASAF Wilaya ya Kishapu, Sospeter Nyamhanga akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga ambaye alikuwa mgeni rasmi kufungua rasmi mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga (hayupo pichani).
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Stephen Magoiga.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...