Naibu
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya akizungumza
na Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji nchini kabla ya Balozi huyo kuzindua
Mkataba wa Huduma kwa Mteja ulioandaliwa na Idara hiyo ambao unalenga kuboresha
zaidi huduma zitolewazo na Uhamiaji ambapo kuanzia sasa Pasipoti zitapatikana
kwa siku tano za kazi mara baada ya mteja kuiomba Makao Makuu Dar es Salaam na
Zanzibar, pia Wateja wa mikoani watapata Pasipoti hizo kwa siku zisizozidi
kumi. Uzinduzi huo umefanyika Makao Makuu ya Idara hiyo, Kurasini jijini Dar es
Salaam. Watatu kushoto (upande wa pili) ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Idara hiyo,
Victoria Lembeli.
Na Humphrey Shao, Globu ya jamii.
Idara ya uhamiaji imezindua mkataba wa huduma kwa wateja ambao
utawawezesha kutoa hati ya kusafiria ndani ya siku tano bila kuchelewa.
Akizungumza na wahabari katika makao makuu ya idara ya uhamiaji jijini
Dar es Salaam,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi
Simba Yahya amesema kuwa kama watumishi wa idara hiyo watashindwa kukidhi
vigezo hivyo walivyojiwekea wananchi wana haki ya kulalamika na kutoa taarifa
katika ngazi za juu.
“Tumejiwekea viwango kuwa wakati wote mtu kama ataomba pasipoti apewe
ndani ya sikutano mkataba huo umeonyesha wajibu wa mtoaji huduma kumuhudumia mteja vile inavyotakikana” amesema
Balozi Yahya.
Ameongeza kuwa kuanzia sasa mteja ni mfalme pindi anapofika katika idara
hiyo kuhitaji hati ya kusafiria na sasa ana fursa ya kulalamika pindi huduma
atakayopata kuwa aitakuwa na radha.Amemaliza kusema kuwa kuwa kuanzia sasa watu wote watapewa huduma kwa
heshima na taadhima kutoka idara ya uhamiaji.
Naibu
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya akikata utepe
kuashiria Uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa Idara ya Uhamiaji. Mkataba
huo ambao unalenga kuimarisha huduma mbalimbali za Idara hiyo pia umeelekeza
kuanzia sasa Hati za Kusafiria (Pasipoti) zitatolewa kwa siku tano za kazi kwa
watakaoomba Makao Makuu Dar es Salaam na Zanzibar, pia Wateja wa mikoani
watapata Pasipoti hizo kwa siku zisizozidi kumi. Wapili kushoto ni Kaimu
Kamishna Jenerali wa Idara hiyo, Victoria Lembeli. Uzinduzi huo umefanyika
Makao Makuu ya Idara hiyo, Kurasini jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, Balozi Simba Yahya akionesha machapisho ya mkataba wa huduma kwa wateja
kati ya Idara ya Uhamiaji na wananchi.
Baadhi ya wananchi waliofika katika halfa ya
uzinduzi wa mkataba huo.
. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba
Yahya katikati akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa idara ya
uhamiaji.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, Balozi Simba Yahya akisalimiana na watendaji wa uhamiaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...