NA HAMZA TEMBA - WMU
Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu leo imewahukumu kifungo cha miaka 20 jela Peter Kabi na Leonida
Loi Kabi ambao ni wanandoa baada ya kukutwa na meno ya tembo 210 yenye uzito wa
kilo 450.6 pamoja na mifupa mitano ya tembo.
Meno hayo yanayodaiwa
kuwa ni sawa na idadi ya tembo 93 waliouwawa yalikutwa nyumbani kwa washtakiwa
hao tarehe 27 Oktoba, 2012 eneo la Kimara Stop Over Jijini Dar es Salaam.
Hakimu Mkazi Mkuu wa
Mahakama hiyo, Huruma Shahidi amesema ametoa hukumu hiyo leo baada ya mahakama
kujiridhisha na ushahidi wa upande wa Jamhuri ukiongozwa na mawakili Paul
Kadushi na Elia Athanas ambao kwa pamoja umewatia hatiani washtakiwa hao.
Amesema katika kosa
la kwanza kila mtuhumiwa atatumikia kifungo cha miaka 15 jela, kosa la pili na
la tatu miaka 20 kila moja na kwamba hukumu hizo zitaenda kwa pamoja.
Watuhumiwa wa Ujangili, Peter
Kabi (wa pili kulia) na mke wake Leonida Loi Kabi (wa tatu kulia)
wakielekea kusomewa mashtaka ya kukutwa na meno 210 na mifupa mitano ya
tembo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam leo,
wote wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.
Mtuhumiwa wa Ujangili, Peter
Kabi (wa pili kulia) akielekea kusomewa mashtaka ya kukutwa na meno 210
na mifupa mitano ya tembo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini
Dar es Salaam leo, mtuhumiwa huyo na mke wake Leonida Loi Kabi (hayuko pichani) wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...