IDADI ndogo ya Watanzania wanaotumia huduma za kibenki kunachangia pakubwa kuchakaa haraka kwa fedha.

Hayo yamesemwa na Meneja Msaidizi wa Benki Kuu, (BoT) , kutoka Kurugenzi ya Huduma za Kibenki, Bw.Abdul M.Dollah, wakati akijibu maswali ya Washiriki wa Warsha ya Waandishi wa habari za Uchumi na Fedha, inayoendelea kwenye ukumbi wa BoT tawi la Zanzibar, leo Machi 30, 2017 waliotaka kujua ni kwa nini fedha za noi zinachakaa haraka hususan shilingi 500 na shilingi 1,000/_

“Ubora wa karatasi zinazotumika kutengenezea noti zetu unalingana, lakini matumizi makubwa ya noti hizo zilizotajwa, zinapita kwenye mikono ya idadi kubwa ya watu na hivyo kupelekea kuchoka haraka.” Alifafanua
Akifafanua zaidi alisema, Idadi ya Watanzania kwa sense iliyofanyika mwaka 2012 ni Milioni 48, lakini kati ya hao ni Watanzania Milioni 4 tu ndio wanatumia huduma za kibenki, (kuwa na akaunti benki), na idadi ya waliosalia, hutunza wenyewe fedha hizo.

Utunzaji mbaya wa fedha na hali ya hewa ya baadhi ya maeneo nchini, huchangia kuchakaa haraka kwa fedha “ Kwa mfano, kule Tanga maeneo ya Lushoto na Kibondo mkoani Kigoma, kutokana na rangi ya udongo wa sehemu hizo, utakuta fedha inachakaa haraka sana, alisema Bw.Dollah.
Akielezea majukumu ya Kurugenzi ya Huduma za Kibenki ya Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), Bw. Dollah alisema, Sheria namba Nne (4) ya BoT, imeipa kurugenzi hii jukumu la kusanifu, kutoa, kusambaza na kuharibu fedha,(noti na sarafu), zilizochakaa.
Meneja Msaidizi wa Benki Kuu, (BoT) , kutoka Kurugenzi ya Huduma za Kibenki, Bw.Abdul M. Dollah, akitoa mada juu ya Huduma za Kibenki  Benki Kuu ya Tanzania.NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
Washiriki wa semina, wakiangalia noti ya Sh. 10,000, ili kutambua kama ni halali au so halali. 
Bw. Abdul M. Dollah, akitoa mada juu ya Huduma za Kibenki.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...