Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nchini Khamis Mwijuma ‘Mwana FA’ amesema kuwa hakuna mpango wowote wa kurejesha kundi la East Coast, bali wana mpango wa kufanya kazi ya pamoja.
Mwana Fa amesema hayo katika mahojiano maalum na globu ya jamii kuhusu mpango wa kundi hilo ambalo lilipata kutamba katika miaka ya tisini.
“Hatuwezi kurudisha kundi la East Coast, ila tuna mpango wa kurekodi nyimbo kati yangu mimi Ay na Gk, watu wanapaswa kujua hivyo kuliko kusikiliza maneno ya watu” amesema Fa .
FA ameseja kuwa ni vigumu kwa sasa kurudisha kundi hilo kwani mfumo wa maisha na muziki umebadilika na ukitaka kurudisha kundi kutahitjai mazungumzo mengi sana.
Aliendelea kusisitiza kuwa bado watendelea kufanya kazi pamoja lakini sio kurudisha kundi kama ilivyokuwa zamani.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...