
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Gabriel Makalla amemkabidhi shilingi milioni moja Bi Fidea Lucas kwa ajili ya kumsaidia matibabu baada ya kumwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana miaka miwili iliyopita.
Msaada huo ni utekelezaji wa ahadi yake Mkuu wa Mkoa huyo aliyoitoa wiki kadhaa zilizopita kwenye kikao cha kusikiliza kero za wananchi, ambapo baada ya kuguswa aliahidi kumsaidia mama huyo hela ya matibabu
Aidha, Mhe.Makalla ameahidi kufuatilia madai yake yote ikiwemo kumsaidia kupata haki zake kwa mwajiri wake na msaada wa kisheria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...