Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Tanzania imeonekana kuwa katika mwenendo mzuri katika mageuzi ya viwanda na kuanza kufanya vizuri katika sekta hiyo kutokana na usimamizi wa Serikali.

Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji  wa REPOA nchini, Dkt. Donald Mmari alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Semina itakayofanyika March 29 na 30 jijini Dar es Salaam itayohusu umuhimu wa taasisi katika maendeleo ya Viwanda nchini.

"Kuna muelekeo mzuri sana katika juhudi za ukuzaji Viwanda nchini, kwani kwa sasa mazingira ni mazuri tofauti na hapo awali,nchi yetu ina umeme wa uhakika jambo ambalo ni la kwanza katika uchumi wa Viwanda" amesema  Dkt. Mmari

Amesema kuwa katika semina hiyo kwa mwaka huu kutakuwa na msemaji kutoka nchini Canada, ambaye ataeleza ni kwa jinsi gani wao wamefanikiwa katika sekta ya Viwanda.

Pia ametaja kuwa wadau wote watakuwa na ajenda moja tu inayofanana kwa ajili ya kusaidia kukua kwa sera ya viwanda ili nchi iweze kupiga hatua.
Mkurugenzi Mtendaji  wa REPOA Tanzania  Dkt. Donald Mmari, akizungumza na waandishi wa habari juu Semina juu ya Maendeleo ya Viwanda nchini
 Waandishi wakiwa katika mkutano huo wakisikiliza kwa makini
Dkt. Alfred Kinyondo akifafanua jambo mbeke ya waandishi wa habari

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...