Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii
Tanzania imeonekana kuwa katika mwenendo mzuri katika mageuzi ya viwanda na kuanza kufanya vizuri katika sekta hiyo kutokana na usimamizi wa Serikali.
Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA nchini, Dkt. Donald Mmari alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Semina itakayofanyika March 29 na 30 jijini Dar es Salaam itayohusu umuhimu wa taasisi katika maendeleo ya Viwanda nchini.
"Kuna muelekeo mzuri sana katika juhudi za ukuzaji Viwanda nchini, kwani kwa sasa mazingira ni mazuri tofauti na hapo awali,nchi yetu ina umeme wa uhakika jambo ambalo ni la kwanza katika uchumi wa Viwanda" amesema Dkt. Mmari
Amesema kuwa katika semina hiyo kwa mwaka huu kutakuwa na msemaji kutoka nchini Canada, ambaye ataeleza ni kwa jinsi gani wao wamefanikiwa katika sekta ya Viwanda.
Pia ametaja kuwa wadau wote watakuwa na ajenda moja tu inayofanana kwa ajili ya kusaidia kukua kwa sera ya viwanda ili nchi iweze kupiga hatua.
Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Tanzania Dkt. Donald Mmari, akizungumza na waandishi wa habari juu Semina juu ya Maendeleo ya Viwanda nchini
Waandishi wakiwa katika mkutano huo wakisikiliza kwa makini
Dkt. Alfred Kinyondo akifafanua jambo mbeke ya waandishi wa habari


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...