Baadhi ya madarasa ya shule ya msingi Tumaini iliyopo kata ya Kashai, wilaya ya Bukoba Mjini ambayo wanafunzi watahamishwa kwa kujenegwa shule nyingene katika eneo la mtaa wa Mafumbo, kata ya Kashai kutokana na usalama baada ya kuwa karibu na eneo la Kiwanja cha Ndege cha Bukoba.
Baadhi ya majengo mapya ya madarasa ya shule mpya ya msingi ya Tumaini, yaliyopo mtaa wa Mafumbo, kata ya Kashai yakiwa kwenye hatua ya mwisho ya ujenzi wake. Shule hii inamadarasa 24 ya kuanzia darasa la kwanza hadi la Saba, na madarasa matatu kati ya hayo ni ya watoto wenye mahitaji maalumu.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Rwambaizi ya Karagwe wakiwa kwenye kiwanja cha ndege cha Bukoba, katika ziara ya mafunzo.
Abiria wakiwasilisha taarifa zao ikiwemo na ukaguzi wa tiketi, kabla ya kupanda ndege ya Auric wakitokea kwenye kiwanja cha ndege cha Bukoba wakielekea Mwanza.
Msimamizi wa Kitengo cha Usalama, Bi. Theodora Myaka wa Kiwanja cha ndege cha Bukoba (kushoto) akimkagua abiria Bi. Jasmindee Dhaliwa, Raia wa Bulgaria huku Afisa Usalama Msaidizi, Bw. Reginald Baraka akiangalia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...