Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau akiongea na waandishi wa habari kuhusu watoto nane wanaokwenda  nchini Israel kwa ajili ya matibabu ya moyo. Hili ni kundi la nne la watoto kwenda kutibiwa nchini humo tangu mwaka 2015 ambapo JKCI ilianza ushirikiano  na Taasisi ya Save Child Heart  ya kuwapeleka wagonjwa nchini Israel hadi sasa watoto 40 wameshatibiwa na wanaendelea vizuri. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma ya Uuguzi   Robert Mallya.
 Baadhi ya wazazi ambao watoto wao wamekwenda nchini Israel kwa ajili ya matibabu ya magonjwa ya moyo wakifuatilia kwa karibu mkutano wa waandishi wa Habarai uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
  Kaimu Mkurugenzi wa Huduma ya Uuguzi  kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akiwaongoza watoto wanaokweda kutibiwa magonjwa ya moyo  nchini Israel kuingia kwenye gari kwa ajili ya kwenda uwanja wa ndege kuanza safari ya kuelekea nchini humo. Serikali kupitia JKCI  kwa kushirikiana na Serikali ya Israel kupitia Taasisi ya Save Child Heart imewapeleka watoto nane (8) nchini humo kwa ajili ya matibabu ya moyo.
 Wataalamu wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) , ndugu na watoto wanaokwenda kutibiwa nchini Israel wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa safari ya watoto hao ya kuelekea nchini humo kwa ajili ya matibabu ya moyo.

Picha na Anna Nkinda - JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...