Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Vikundi mbalimbali vya Jogging viliweza kufanya mazoezi kwa pamoja kwa mbio zilizoanzia Uwanja wa Taifa na kumalizikia viwanja vya Mwembe Yanga na kuhamasisha ushirikiano baina yao.

Mbio hizo zilizofanyika jana, vilikutanisha vikundi zaidi ya 15 kutoka sehemu mbalimbali za wilaya ya Temeke pamoja na baadhi kutoka wilaya ya Kinondoni ikiwa ni kuunga mkono katila jitihada za ushirikiano baina yao.

Mwenyeji wa Mbio hizo Kikundi cha Dar Jogging kutoka maeneo ya Chang'ombe kiliwaalika vikundi vingine ikiwa ni moja ya malengo ya kujenga ushirikiano baina yao ikiwemo kujihusisha na masuala ya upatu (saccoss).

Mwenyekiti wa umoja wa vikundi hivyo ujulikanao kama Temeke Jogging Association (TEJA) Mussa Mtulia amesema kuwa vikundi hivyo vinatakiwa kushirikiana kwa njia mbalimbali ili kuweza kujiwezesha kiuchumi na zaidi kuanzishwa kwa upatu baina yao ni mwanzo mzuri wa maendeleo.
 Mwenyekiti wa umoja wa vikundi  Temeke Jogging Association (TEJA) Mussa Mtulia akikabidhi pesa taslimu kiasi cha shillingi laki sabai (700,000) zilizopatikana katika mchezo wa upatu unaochezwa na vikundi hivyo vya Jogging akishuhudiwa na wajumbe wengine kutoka umoja wa vikundi hivyo. 
Wanachama wa kikundi cha Dar Jogging wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa mbio hizo.

Vikundi vya Jogging wakiwa katika mazoezi.Picha na Zainab Nyamka.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...