Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete (mwenye kanzu) akiwa na wananchi wa jimbo hilo wakikagua `Bwawa la Umwangiliaji la Msoga 

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete,ametembelea eneo la Chalinze Mzee lilokumbwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika jimbo hilo na kusababisha madhara ya nyumba kubomoka na nyumba 9 kusombwa na maji na kusababisha zaidi ya kaya 20 kukosa pakulala.

Akizungumza Ridhiwani,ametaja  maeneo yaliyokumbwa na  mafuriko ni Chalinze Mzee,Bwawa la umwangiliaji la Msoga ambalo limetoboka na shule ya Sekondari ya Imperial.

Aidha,amesema kuwa madhara makubwa yaliosababishwa na mafuriko hayo ni kuharibika kwa mashamba,nyumba za wananchi kuharibika na kusabbishwa wananchi kukosa pa kulala,na ameongeza kuwa kwasasa wananchi hao wanahitaji msaada. 

Ridhiwani ametoa pole kwa wakazi hao na kuwaomba kuwa vumilivu katika kipindi hiki.
 Baadhi ya Nyumba katika eneo la Chalinze Mzee zikiwa zimearibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
 Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete akiangalia madhara yaliosababishwa na mafuriko katika jimbo hilo la Chalinze.
 wakazi wa chalinze wakiangalia nyumba zao zilizobomoka kutokana na mafuriko.
 Sehemu ya bwawa la umwangiliaji la Msoga liloaribiwa na mafuriko na kupasua kingo za bwawa hilo.
 Moja ya Nyumba iliyobomoka kutoka na mvua zinazoendelea kuonyesha katika eneo la Chalinze.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...