Kwa mara nyingine tena upelelezi dhidi kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayomkabili Rais wa  Klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange Kaburu umedaiwa kuwa bado kukamilika na kwamba kuna nyaraka mbalimbali zimepelekwa kwa mtaalamu wa maandishi.

Wakili wa serikali, Eatazia Wilson amedai hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa, pindi kesi hiyo imekuja kwaajili ya kutajwa na kudai bado wanasubiri ripoti ya polisi.

Kufuatia taarifa hiyo, Hakimu Nongwa aliutaka upande wa jamuhuri kujitahidi kuharakisha upelelezi kwasababu washtakiwa wapo ndani na kwamba
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 8 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Aveva na Kaburu  wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...