Marehemu Profesa Joseph  Nagu,  aliyekuwa Mhadhiri katika Chuo Kikuu Mzumbe, alikuwa  mume wa Mbunge wa Hanang- Mhe. Mary Nagu ambaye pia alikuwa Waziri katika serikali ya awamu ya tatu na ya nne. Marehemu Prof. Nagu ni baba wa Dr. Tumaini, Neema na Deogratias. 
Tunapenda kuwajulisha kuwa Marehemu atapumzishwa katika nyumba yake ya milele nyumbani kwake Endasaki Wilaya ya Hanang siku ya Alhamisi tarehe 3/8/2017 
Leo saa kumi jioni Ibada ya kumuaga Marehemu imefanyika katika kanisa Katoliki St Peters Oysterbay jijini Dar es salaam kabla ya mwili kupelekwa kulala nyumbani kwake Regent Estate Mikocheni tayari kusafirishwa siku ya tarehe 02/07/2017 kuelekea Manyara, Hanang', Kijiji cha Endasaki. 

Raha ya milele umpe ee Bwanana na mwanga wa milele umwangazie.
Apumzike kwa Amani Mzee wetu Prof Joseph Nagu - AMEN.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...