Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi  Juliana Pallangyo leo tarehe 24 Agosti, 2017 amefanya kikao cha kazi na watendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO mkoa wa Mtwara mjini Mtwara lengo likiwa ni kujadili mafanikio na changamoto za utendaji kazi. Dkt. Pallangyo amewataka watendaji hao  kuwa wabunifu kwenye ukusanyaji wa mapato pamoja na kuwasilisha  taarifa za utekelezaji za kila baada ya miezi mitatu.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi  Juliana Pallangyo (mbele) akiongoza kikao kilichoshirikisha watendaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO mkoa wa Mtwara mjini Mtwara
 Sehemu ya watendaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO- Mtwara wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi  Juliana Pallangyo (hayupo pichani) katika kikao hicho.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi  Juliana Pallangyo akisisitiza jambo katika kikao hicho
 Afisa Rasilimaliwatu wa Kanda ya Kusini, Bonus Msuha (kushoto) akieleza jambo katika kikao hicho. Kulia ni Meneja wa TANESCO-Mtwara Mhandisi  Aziz Salum
Sehemu ya watendaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO- Mtwara na Wizara ya Nishati na Madini  wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi  Juliana Pallangyo (hayupo pichani) katika kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...