Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BAADA ya kufanyika kwa makosa wakati wa utengenezaji wa Ngao ya Jamii, Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini 'TFF'  imetengeneza Ngao mpya kwa ajili ya klabu ya Simba baada ya ile ya awali kukosewa kuandikwa.


Klabu ya Simba ilifanikiwa kushinda katika mchezo wa Ngao ya Jamii August 23, 2017 baada ya kuifunga kwa mikwaju ya penati 5-4 mahasimu wao Yanga na kukabidhiwa Ngao ya Jamii ambayo ilikuwa na makosa ya kiuandishi.


Ngao ya Jamii ya awali iliyokabidhiwa kwa washindi hao wa mwaka 2017 Simba iliandikwa ‘Community Sheild’ badala ya ‘Community Shield’ kitu ambacho kilizua mijadala kwenye mitandao ya kijamii na kupelekea TFF kuomba radhi kwa wanafamilia wa mpira wa miguu nchini na kuahidi tukio kama hilo halitojirudia tena.

Afisa habari wa TFF Alfred Lucas ameionesha Ngao ya Jamii iliyofanyiwa marekebisho itakabidhiwa  kwa Simba siku ya mechi ya ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Azam FC.


Afisa habari wa TFF Alfred Lucas akionesha Ngao ya Jami mpya iliyofanyiwa marekebisho na tayari kukabidhiwa kwa Klabu ya Simba  siku ya mechi ya ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Azam FC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...