SERIKALI imesema inaanza kutoa leseni mpya za machapisho mbalimbali ikiwemo magazeti na majarida yote nchini ikiwa ni utekelezaji wa matakwa ya kifungu cha 5(e) cha Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 unaokwenda pamoja na Kanuni ya 7 ya Kanuni za Sheria ya Huduma za Habari za mwaka 2017 zilizochapishwa kwa mujibu wa tangazo la Serikali na 18 la Februari 3, 2017.

Akizungumza katika Mkutano na Wanaandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo, Mkurugenzi Mkuu, Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amesema kuwa utoaji huo wa leseni kwa machapisho yote umeanza rasmi leo Agosti 23, 2017 na utafikia tamati Octoba 15, 2017 na magazeti yote yahakikishe yanakamilisha taratibu ya kupatia leseni mpya kwa kipindi hicho, na baada ya muda huo hawataruhusiwa kuyachapisha kwani watakuwa wanatenda kosa kisheria.



Dkt. Abbas amesema, kwa mujibu wa sheria, utaratibu huu wa sasa unafuta mfumo wa awali wa utoaji wa Hati za Usajili wa magazeti na majarida uliokuwa ukitumika kwa mujibu awali kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.


Fomu za maombi, akaunti ya kulipia pamoja na orodha ya nyaraka zinazohitajika kwa ajili ya usajili huo, vinapatikana kuanzia saa katika ofisi za Idara ya Habari - MAELEZO za jijini Dar es salaam na Dodoma au katika sehemu ya "Huduma Zetu" katika tovuti ya Idara hiyo BOFYA HAPA.
Mkurugenzi Mkuu, Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas akizungumza katika Mkutano na Wanaandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...