Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo wamefanya ziara katika miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kwa lengo la kujua Maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo.
 
Miradi iliyotembelewa ni Barabara ya Watani kwa Jongo Kata ya Makurumla ambayo ina Urefu wa kilomita 1 na inajengwa kwa kiwango cha changarawe kwa kutumia fedha za Ndani (own source), Barabara ya Ubungo Msewe kutokea  Kimara Baruti yenye urefu wa Kilomita 2.6 inasimamiwa na TAN ROADS, Pia Barabara ya Kifuru – Msigani yenye urefu wa kilomita 4.0 ambayo ina simamiwa na TAN ROAD na inajengwa kwa kiwango cha lami.

Wajumbe wa bodi ya Barabara hiyo wamedhamiria kuhakikisha miradi iliyopangwa  inatekelezwa kwa wakati na kwa ubora ili kuboresha miundo mbinu ambayo itawanufaisha na kuwaletea maendeleo wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Wajumbe hao kwa Upande wa Manispaa ya Ubungo ni Mhe. Mbunge wa viti maalumu Suzan Lymo, Mkururugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo, Katibu tawala wa Wilaya Ndg James  Mkumbo  na Wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa ni ziara ya kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. Leo Agosti 14
Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua daraja lililopo kwenye barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa ni ziara ya kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. 
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (Kulia) akiwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James Mkumbo wakati wa ziara ya Wajumbe wa bodi ya barabara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakikagua barabara ya Watani kwa Jongo katika Kata ya Makurumla,leo Agosti 14


Muonekano wa Barabara ya Kifuru-Msigani ikiwa katika hatua za awali za ujenzi,leo Agosti 14.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...