Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi amepokea rarmi Rasimu ya Mkakati wa kukabiliana na Changamoto za Matumizi bora ya Ardhi Nchini na kutaja Teknolojia kuwa ni changamoto inayokabili mpango wa matumizi bora ya ardhi inayopelekea kulegalega kwa upangaji, upimaji na umikilishaji wa Ardhi.

Waziri Lukuvi ameyasema hayo mjini Morogoro wakati alipokuwa akipokea rasimu ya mkakati wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya ardhi nchini, iliyoonesha na kuainisha mapendekezo katika uandaaji,usimamizi na utekelezaji.

“Tunahitaji teknolojia rahisi ambayo hata ninyi mkondoka serikali inaweza kuhimili, hatupendi mtuambukize teknolojia ambayo itakuwa ni ngumu kwetu, kwakuwa serikali inapopanga gharama kubwa zinajitokeza kwenye picha za anga na zile za chini,” alisema Lukuvi.

Lukuvi alisema kuwa kuhusu fedha si tatizo lakini ukosefu wa teknolojia ndio tatizo kubwa zaidi,hivyo ni vizuri kuyatazama haya mashirika yasiyo ya kiserikali tushirikiane nayo ili yaweze kuangalia ni teknolojia gani rahisi itakayoweza kupunguza gharama za upimaji na upangaji wa ardhi vijijini baada ya kusubiri ndege za anga ambazo ni gharama kubwa.

Aliongeza kuwa Serikali inapenda kuwa na uratibu wa haraka, ulio rahisi ambao wananchi wanaweza kupanga maeneo yao na kuongeza, lakini pia kuondokana na migogoro ya Ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akifungua rasmi mkutano kwa ajili ya kusikiliza na kupokea Rasimu ya Mkakati wa Kukabiliana na Changamoto za Matumizi Bora ya Ardhi Nchini, mjini Morogoro.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe akitoa maelezo juu ya mkutano huo na kuonesha namna gani itakavyoweza kumaliza migogoro ya Ardhi Nchini.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...