Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Dkt. James Wakibara (wa tatu kushoto, mstari wa mbele ) akiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka hiyo, Imani Nkuwi (kushoto kweke) na viongozi pamoja wafanyakazi wa Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha. Lengo la ziara hiyo ilikua kuona na kukagua shughuli zinazofanywa na kikosi hicho kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wake.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Dkt. James Wakibara (katikati) akisikiliza hoja mbalimbali kutoka kwa watumishi wa KDU alipotembelea ofisi zao hivi karibuni. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi wa Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka hiyo, Imani Nkuwi (kulia) na Mkuu wa Kikosi hicho Kanda ya Kaskazini, Ndugu Mkeni (kushoto). 
 Askari wa KDU Kanda ya Kaskazini wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA, Dkt. James Wakibara wakati akitoa maelekezo mbalimbali ya kuboresha utendaji kazi wa kikosi hicho.
Baadhi ya watumishi na Askari wa KDU Kanda ya Kaskazini wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA (hayupo pichani).
Wafanyakazi na Askari wa KDU Kanda ya Kaskazini wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA, Dkt. James Wakibara wakati wa mkutano huo. (PICHA NA TAWA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...