Na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW
Serikali imeadhimia kuwa Sera ya Maendeleo ya Jamii ya mwaka 1996, inatekelezwa kikamilifu na inafuatilia utekelezaji wa Sera hiyo katika ngazi ya mikoa, Wilaya, Kata na Vijiji mbalimbali hapa nchini.
Akiongea na wananchi wa Kijiji cha Manghangu, kilichoko Kata ya Vinghawe Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bw. Patrick Golwike amesema Sera hiyo imeweka wazi kuwa wananchi ndiyo kitovu cha maendeleo maana ushiriki wao unatoa dhamana thabiti ya maendeleo na ustawi wa wananchi katika ngazi mbalimbali.
Bw. Patrick Golwike ametanabaisha kuwa lengo la kufika katika Kijiji hicho ni kushirikiana na wananchi kufanya kazi za maendeleo kwa vitendo.
“Kazi ya kuhamsha ari iliyobuniwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalenga kuhamasisha wananchi kushiriki katika kuibua miradi, kupanga, kutekeleza na kusimamia shughuli za maendeleo kwa kutumia rasilimali zilipo katika mazingira yao ili kujiletea maendeleo yao” alisema Bw. Golwike.
Kwa upande wake Mratibu wa masuala ya Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI Bibi Mwajina Lipinga, alisema kuwa mradi wa ujenzi wa lambo la maji, na ushiriki wa wananchi katika kazi za kujitolea utakuwa chachu kwa vijana kuhamsha ari ya kujitolea na kuchangia maendeleo ya vijiji na Taifa.
Sehemu ya vijana wa Kijiji cha Manghungu, Kata ya Vinghawe Halmashauri ya Mpwapwa mkoani Dodoma wakishiriki kazi ya kuchimba Lambo kwa kutumia nguvu zao wenyewe.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii Bw. Patrick Golwike akishiriki kuchimbua eneo la Lambo la Kijiji cha Manghungu, Kata ya Vinghawe Halmashauri ya Mpwapwa mkoani Dodoma.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Bw. Mohamed Maje akiweka mchanga kwenye ndoo katika zoezi la uchimbaji wa Lambo Kijijini cha Manghungu.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Manghungu, kata ya Vinghawe Halmashauri ya Mpwapwa mkoani Dodoma wakishiriki kazi ya kuchimba Lambo kwa kutumia nguvu zao wenyewe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...