Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe akihutubia wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Kituo cha Madini na Kijiosayansi cha Afrika (AMGC) jijini Dar es Salaam baada ya Kituo hicho kutimiza miaka 40 tangu kuanzishwa kwake.
Mwakilishi Mkazi wa Masuala ya Uchumi kutoka Ubalozi wa China, Lin Zhiyong mmoja wa wafadhili wa AMGC akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo, Ibrahim Shaddad kwa ushirikiano mwema uliopo kati yao.
Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania, Monica Patricio Clemente akichangia hoja katika Mkutano wa Baraza la Uongozi wa AMGC jijini Dar es salaam.
Wajumbe mbalimbali wa Mkutano wa Baraza la Uongozi wa AMGC wakiwa katika kikao cha 37 nchini Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...