Violet Brown
Emma Morano 

Violet Brown aliyezaliwa tarehe 10 March 1900  na kufariki dunia  jana Ijumaa tarehe 15 September 2017 ni mwanamke wa Jamaica ambaye hadi mauti yanamkuta ndiye aliyethibitishwa kuwa mtu mwenye umri mkubwa kuliko watu wote duniani kufuatia kifo cha aliyekuwa anashika rekodi hi mwanamama wa Italia Emma Morano  aliyezaliwa tarehe 29 November 1899  na kufa tarehe 15 April 2017  akiwa na umri wa miaka 117 na siku 189.


Mama Violet pamoja na Nabi Tajima (pichani kulia) wa Japan  (aliyezaliwa   tarehe 4 August 1900)   walikuwa watu wawili wa mwisho duniani waliojulikana kuwa walizaliwa katika karne ya 19. Hivyo rekodi hiyo ya uhai mrefu inashikiliwa sasa na Mama Tajima.


Akiwa mmoja wa watoto wane wa mzee John Mosse, mchemsha sukari katika kiwanda kwenye shamba la  miwa, na mama Elizabeth Riley, Mama Violet aliolewa na Bw. Augustus Gaynor Brown na wakajaaliwa kupata jumla ya watoto sita, wane wao  wakiwa hai wakati wa kifo chake jana.

Kwenye Mahojiano Mama Violet alisema yeye alikuwa na afya bora kuliko wanawe na hakuwa na maradhi yoyote. Alipoulizwa siri ya uhai wake mrefu alisema hakuna siri kwa kweli.
“Haki ya nani tena ni kweli watu wakiniuliza nakula nini na kunywa nini, nawaambia nakula kila kitu isipokuwa kitomoto na kuku. Pia sinywi pombe na    y ale mambo Fulani (ganja) situmii…”alisema Mama Violet.

 parent.[15] Death Brown died on 15 September 2017 at a hospital in Montego Bay, Saint James Parish, of heart failure complicated by dehydration at the age of 117.[16]

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...