Uzalendo limekuwa neno kuu katika siku za karibuni. Na wengi wetu tunatafsiri kama ni kuipenda na kuiweka Nchi yako mbele. Lakini sifa nyingine muhimu sana ya uzalendo ni kujitolea kwa faida au maendeleo ya wengi.
Salasala Vision Group ( SVG) iliasisiwa miaka 5 iliyopita na wakazi wachache wa Salasala Kilimahewa lengo likiwa ni kisaidia masuala ya ulinzi, mazingira, miundombinu, michezo na kuchochea maendeleo ya wanachama wake.
Hadi leo SVG imepanda miti zaidi ya 10,000, imetengeneza barabara za mitaa pamoja na kurekebisha barabara kuu, imetoa msaada vitendea kazi kwa polisi, kutengeneza viwanja vya michezo na pia kununua aridhi kwa wanachama wake zaidi ya hekari 250 huko Bagamoyo.
Wiki hii kwa mwaliko wa Spika wa Bunge SVG imetembelea Bungeni na kisha kucheza mechi na timu ya Bunge na kuibuka na ushindi wa bao 2 - 1.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...