Na. Eliphace Marwa - Maelezo

Serikali imeingiza nchini jumla ya tani elfu 32 za mbolea ya kukuzia pamoja na tani elfu 23 za mbolea ya kupandia kupitia mfumo mpya wa uagizaji wa mbolea kwa pamoja, lengo likiwa ni kudhibiti bei kwa kuzingatia bei elekezi.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam wakati zoezi la upakuaji wa mbolea hiyo likiendelea Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Ubora wa Mbolea Tanzania(TFRA) Bw. Lazaro Kitandu amesema kuwa mpaka sasa jumla ya tani elfu 55 za mbolea zimewasili nchini.

Hii ni awamu ya kwanza ya kuingiza mbolea nchini kupitia mfumo mpya ya uagizaji mbolea kwapamoja ambapo kampuni ya OCP S.A ya nchini Morocco imeingiza jumla ya tani elfu 23 za mbolea ya kupandia na Kampuni ya Premium Agro Chem imeingiza tani elfu 32 za mbolea ya kukuzia.

“Mpaka sasa zoezi la kupakua mbolea ya kupandia (DAP) tani elfu 23 linaendelea vizuri na mara baada ya kumaliza kupakua mbolea hii tutaanza zoezi la kupakua mbolea ya kukuzia (UREA) ambayo ni tani elfu 32,” alisema Bw. Kitandu.
Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Ubora wa Mbolea Tanzania(TFRA) Bw. Lazaro Kitandu (katikati) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wakati zoezi la upakuaji wa mbolea ya kupandia ukiendelea katika bandari ya Dar es Salaam mapema hii leo. 
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari nchini wakiendelea na zoezi la upakiaji wa mbolea ya kupandia tani elfu 23 tayari kwenda kwa wakulima mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari nchini wakiendelea na zoezi la kufunga mbolea ya kupandia katika mifuko tayari kwa kupakiwa na kusafirishwa kwenda kwa wakulima.Picha na Eliphace Marwa - Maelezo



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...