Jovina Bujulu-MAELEZO.
Sekta ya kilimo nchini ni kitovu cha maendeleo ya viwanda kwa kutoa masoko na malighafi za viwandani ambapo inaajiri Watanzania wengi takribani zaidi ya asilimia 67.
Katika utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo, Serikali inaendelea kuimarisha mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya kilimo ikiwemo kuimarisha masoko ya kilimo ili sekta hiyo iendelee kuwa na tija kwa wakulimananchi na taifa kwa ujumla.
Hivi karibuni Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ilitangaza kufuta ada na tozo mbalimbali katika baadhi ya mazao ya biashara ili kumpa unafuu mkulima wakati wa kuuza mazao yake.
Hatua hiyo ni mwanzo mzuri wa kuimarisha sekta hiyo hasa wakati huu ambapo Serikali ya Awamu ya Tano imetangaza nia yake ya kuimarisha uchumi wa kati na viwanda.
Serikali iliamua kufuta na kupunguza ada na tozo imedhamiria kumaliza kero na kilio cha muda mrefu cha wakulima ambao wamekuwa wakilalamikia tozo hizo kwa madai kuwa zinawanyonya.
Aidha, uamuzi huo unategemea kuwapunguzia mzigo mkubwa wa malipo ambao umekuwa ukiwaelemea wakulima hao, hivyo kuwapa unafuu mkubwa na kuwapatia faida.
Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2017/18, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba alizitaja baadhi ya tozo zilizofutwa katika zao la tumbaku kuwa ni mchango wa ushirika wa mkoa, mchango kwa ajili ya gharama za masoko ya ushirika na chama cha msingi cha ushirika, dhamana ya benki kuu ya Tanzania na fomu ya maombi ya leseni za tumbaku.
Ada na tozo nyingine zilizotajwa kuwa ni kodi ya leseni ya kununua tumbaku kavu na mbichi kiwandani, leseni ya kuuza tumbaku nje ya nchi na tozo ya Baraza la Tumbaku.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...