KIASI cha shilingi milioni tatu na laki saba, Hati za wateja tofautitofauti pamoja na nyaraka mbalimbali za ofisi ya mawakili ya Prime Attorney advocate zilizopo upanga jijini Dar es Salaam zaibwa na watu wasiojulikana wakati walipovamia ofisi hiyo majira ya saa tisa na nusu usiku.

Hayo yamesemwa na wakili, Asia Charles akizungumza kwa niaba ya Wakili Hudson Ndusyepo wakati akizungumza na Michuzi Blog leo amesema kuwa “Ni kweli Majambazi hao walifanikiwa kuvunja milango ya ghorofa ya kwanza na ya pili hawakuchukua kitu chochote na wakafanikiwa kupanda mpaka ghorofa ya tatu upande wa kushoto  waliingia ofisi ya Mhasibu na kufanikiwa kuchukua kabati binafsi (Self) ambalo lilikuwa na Nyaraka za Ofisi, pesa shilingi milioni Tatu na laki saba pamoja na Nyaraka mbalimbali za Wateja".

Amesema kuwa Watu hao wamecheza zaidi na Vitasa vya Milango na kufanikiwa kufungua Milango na kuiba Kabati Binafsi (Self) walilokuwa wanalitaka.

Asia maesema kuwa Mlinzi alieleza kuwa walipofika katika ofisi hizo alijitahidi kuwazuia lakini wakamshinda kutokana na kumzidi nguvu pamoja na uwingi wao, pia mlizi amesema aliwaambia kuwa walimwambia asiongee kitu chochote na wakamuamlisha awapeleke wanakotaka na baadae baada ya kufika wakamziba mdomo na Plasta Nyeusi ili asiweze kupiga kelele.

 "Tunasubiri  Uchunguzi wa Polisi Ukamilike ndio tunaweza tukatoa taarifa kamili" Amesema Asia. Wakili, Asia Charles akizungumza na Mwandishi wa Michuzi Blog jijini Dar es Salaam leo amesema kuwa Kiasi cha shilingi Milioni Tatu pamoja na Nyaraza za ofisi ya Prime Attorney advocate  pamoja hati mbalimbali za wajeja wao zimeibwa na watu wasiojulikana walipovamia Ofisi hiyo Usiku wa Kuamkia leo Upanga jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Sehemu zilizoharibiwa na watu waliovamia Ofisi ya Prime Attorney advocate iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam na kuchukua Nyaraka za ofisi hiyo zilizokuwa kwenye kabati binafsi (Self). 
Baadhi ya haribifu uliotokea katika ofisi ya Prime Attorney advocate.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...