Kampuni ya Zuku imezindua huduma ya Intaneti yenye uwezo mkubwa wa kuweza kufanya kazi kwa vitu vitatu kwa wakati mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Afisa Mtendaji wa Zuku Fiber, Thomos Hintze amesema kuwa Zuku Fiber inawezo mkubwa kuliko mitandao mengine iliyopo nchini.

Amesema kuwa wamejipanga kutokana na kampuni hiyo kuwa na miundombinu inayojitosheleza ambapo mtu akilipia anapata huduma muda huo huo

Hata hivyo amesema kifurushi cha Zuku fiber triple Play 100 mbps kimeundwa ili kukidhi mahitaji ya mtandaoni kama video fupi, sinema , michezo ya kuigiza na video za mawasiliano.

Hintz amesema kuwa gharama za mtandao huo ni sh .79,000 ambapo Mteja anapoanza  kutumia uwezo wake ni uleule mpaka mwisho.

Amesema kampuni hiyo imekwenda mbali baadhi ya nchi za Afrika ambazo ni Zambia, Malawi, Uganda pamoja na Kenya.

Afisa Mtendaji wa Zuku Fiber, Mhandisi Thomos Hintze akizungumza na waandishi katika uzinduzi wa Intaneti  Fiber iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Kulia ni Meneja wa Zuku Fiber Thomas Wenanga  pamoja na Mkuu wa kitengo cha Fiber, Michael Debaly 
Meneja Uendashaji wa Zuku Fiber, Mcharo Mlaki akizungumza katika uzinduzi wa huduma ya Intaneti iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Zuku Fiber, Mhandisi Thomos Hintze akiwa na watendaji wa kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...