Na Yeremias  Ngerangera, Namtumbo

Athmani  Amani  mkazi wa kijiji  cha Naikesi  kata ya kitanda  wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma  anawaomba  watanzania  kumsaidia  fedha  za kugharimia  matibabu  ya mtoto  wake  Shaziri  Athmani (12) anayesumbuliwa  na tatizo  la moyo kuwa  mkubwa.

Mtoto  Shaziri  Athamani  ni mwanafunzi  wa darasa  la nne  shule  ya msingi Naikesi  iliyopo  kata ya Kitanda  wilayani Namtumbo  awali  alikuwa anasumbuliwa  na kuvimba  miguu  hali iliyokuwa  inamkosesha  masomo  yake  darasani  mara kwa  mara kuanzia  mwaka  2016.
Mwaka  huo  huo  mwezi  Septemba  baba yake  alilazimika kumpeleka  Hospitali  ya Mkoa  Songea  kuangalia tatizo  la kuvimba  kwa  miguu  ya mtoto huyo  na  baada ya kupata  vipimo  wakashauriwa  kuenda  Hospitali  ya  Peramiho  .

Bwana  Athamani  alidai  kuwa  hakuwa  na fedha  za kumpeleka  mtoto  peramiho  kwa  kipindi  hicho  na badala yake  alirudi  naye  nyumbani  Naikesi  kwenda  kuuza  mifugo  lakini fedha hizo  hazikumwezesha  kukidhi  mahitaji  ya  kumtibu  mwanoa katika  Hospitali  ya  Peramiho  baada  ya  kufika  katika  Hospitali  hiyo  na kumaliza  fedha  yake  yote  aliyokuwa  nayo  katika  vipimo  pekee .

Baada  ya kupatiwa  vipimo  na  kubaini  Tatizo la  mwanae  alirudi  na mwanae  mpaka  kijijini  kwake  kujipanga  upya  kwa  ajili  ya  matibabu ya  mwanae  na  kujitahidi  kwa kile  anachokipata  anunue  dawa  kwa  ajili  ya  mwanae  huyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...