MKUU wa wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani,Gilberto Sanga amekubali kuwa Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha baba wa taifa,Julius Nyerere yatakayofanyika Oktoba 14,2017 katika kijiji cha wasanii Mwanzega wilayani hapa.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Cassim Taalib alisema jana kuwa katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya atagawa nyumba 18 zilizojengwa na wanachama wa mtandao kwa njia ya kuchangiana na atakabidhi alama 55 kwa wanachama.

Alisema katika maadhimisho hayo ambayo SHIWATA huadhimisha siku hiyo kila mwaka kwa matukio mbalimbali mwaka jana walikabidhi fedha kwa watu waliopata maafa ya tetemeko la ardhi mkoa wa Kagera.

Taalib alisema SHIWATA ambayo mpaka sasa imekwisha kabidhi nyumba 268 zilizojengwa kwa njia ya kuchangiana pia imekuwa ikiendesha matamasha ya wasanii mbalimbali kuonesha vipaji vyao.

Alisema Julai mwaka huu SHIWATA iliendesha tamasha la wasanii wote na Desemba mwaka huu kutakuwa na mashindano ya soka ambayo yalianza mwaka jana na timu ya maveterani ya Kitunda iliibuka kuwa mabingwa kati ya timu sita zilizoshindana.

Katika hatua nyingine wanachama wa SHIWATA ambao mashamba yao yanachukuliwa na serikali kwa ajili ya kujenga viwanda wameazimia kutafuta mashamba mengine kando kando ya reli ya Kati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...