Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda pamoja na Mkuu wa wilaya ya Kigamboni , Hashim Mgandilwa, vinongonzi mbalimbali  wakiangaria ramani ya eneo maalumu lililotengwa Kigamboni kwa ajili ya Showroom zote za Magari jijini Dar es Salaam.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda jana alitembelea na kukagua Maendeleo ya ujenzi wa miundombinu  kwaajili ya Showroom zote za Magari kwenye eneo Maalumu lililotengwa Kigamboni.

RC Makonda ameongozana na viongozi wa Taasisi mbalimbali ikiwemo TRA, SUMATRA, NSSF, Bank ya watu wa Zanzibar pamoja na Jeshi la Polis na Jeshi la Zimamoto na uokoaji ambao wameenda kuonyeshwa maeneo yaliyotengwa kwaajili ya Ujenzi wa Ofisi.

Makonda amesema kuwa lengo kuhamishia Showroom Kigamboni ni kufanya Kigamboni kuwa soko la Magari Africa, kuwapa Wananchi fursa ya kuchagua gari analotaka kwenye  eneo moja, kuiwezesha Serikali kupata mapato na kupunguza wizi wa magari.

Akiwa kwenye eneo hilo ameshuhudia ujenzi wa miundombinu ya Barabara, Madaraja, Umeme na Maji ikienda kwa kasi kubwa.
Tayari baadhi ya Taasisi na wenye Showroom waliokabidhiwa maeneo wameanza kujenga ili kuhakikisha ifikapo January Mosi wanakuwa wamehamisha Showroom zao.

Ndani ya eneo hilo kutakuwa na ofisi za Taasisi zote zinazohusiana na biashara ya Magari ikiwemo TRA, TPA, SUMATRA, Bank, NSSF,Bima, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto na uokoaji, Garage, Sheli na Wauzaji wa Vipuri vya Magari.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda  pamoja na Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa,viongonzi mbalimbali  wakikagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu  katika eneo maalumu lililotengwa  kwaajili ya Showroom zote za Magari.(Picha na Emmanuel Massaka,Glob ya jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...