Watoto wa marehemu mzee Raphael Mlondoye Msyaliha wa Mbeya mjini wanasikitika kutangaza kifo cha baba yao mpendwa mzee Raphael Mlondoye Msyaliha aliyefariki usiku wa kuamkia tarehe 10 Oktoba 2017 katika Hospital ya Rufaa.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu Mbeya mjini karibu na hospitali ya Rufaa. Habari ziwafikie watoto wote wa marehemu, wana ukoo wote wa Msyaliha,Shonza,Shura,Mwamlima,Paza,sijabaje,halinga,mgala,ntenga,Ntengwi,Mwashambwa,Njeje na Mwawalo , ndugu wote na jamaa wa marehemu wateja na wadau wote wa Victoria Engeneering.

Mazishi yamepangwa kufanyika Mbozi kijiji cha Igale kata ya Iyula siku ya Alhamis tarehe 12 mwezi wa 10 2017.
Mwenyezi MUNGU ailaze roho ya marehemu baba yetu mahala pema peponi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mwenyezi MUNGU aiweke roho Marehemu baba yet mpendwa mahala pema peponi.tutakumbuka daima kwa upendo wako.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...