NA K-VIS
BLOG/KHALFAN SAID, Mtwara.
WAHANDISI na mafundi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),
wanapambana usiku na mchana kuzifanyia matengenezo mashine za kufua umeme, ili
kuondoa tatizo la kukosekana kwa umeme kwa vipindi virefu kila siku kwenye
mikoa ya Mtwara na Lindi.
Akizungumza
mjini hapa leo Oktoba 14, 2017, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,
anayeshughulikia Uzalishaji, Mhandisi Kaitwa Bashaija, (pichani juu), amesema kwa sasa Wahandisi
na mafundi wa shirika hilo wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana ili
kutengeneza mitambo hiyo na hivyo kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi kwa
haraka.
K-VIS BLOG ilishuhudia mafundi hao wakifanyakazi ya
kurekebisha mitambo hiyo katika kituo cha kuzalisha umeme wa kutumia gesi
asilia mkoani Mtwara leo Oktoba 14, 2017.
“Mitambo hii ina kiasi cha mika 10 tangu ifungwe, na kadiri
miaka inavyokweda ndivyo ongezeko la uhitaji wa umeme hususan mkoani Mtwara
linazidi kuongezeka kutokana na kukua kwa shughuli za kiuchumi,” Alisema
Mhandisi Bashaija.
Alisema, miaka michache iliyopita baadhi ya mitambo
iliweza kuzimwa na bado hali ya umeme ilikuwa imara.Wiki iliyopita Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani
aliagiza TANESCO kufanya juhudi za ziada kuhakikisha tatizo la umeme mkoani
Mtwara na Lindi linapatiwa ufumbuzi wa haraka.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Mhandisi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akifanyia matengenezo moja ya mashine za kufua umeme kwenye kituo cha kufua umeme Mtwara, leo Oktoba 14, 2017
Wahandisi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akifanyia matengenezo moja ya mashine za kufua umeme kwenye kituo cha kufua umeme Mtwara, leo Oktoba 14, 2017
Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa
kutumia gesi asilia cha Mtwara, Mhandisi Mkulungwa Chinumba,
akizungumzia hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha tatizo hilo
linapatiwa ufumbuzi wa haraka. Kulia ni Mhandisi Bashaija.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...