Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim, Bwana Stanley Kafu akimkabidhi vitanda Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge
 ikiwa benki ya Exim ina Mradi unalenga kusaidia upungufu wa vitanda katika hospitali hapa nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro and vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini.Mashuhuda wa msaada huo unavyotolewa ni Mwenyekiti wa bodi wa hospitali Dodoma
 Job Lusinde na Daktari mkuu wa Mkoa wa Caroline Damian.
 Daktari wa Mkoa wa Dodoma,Caroline Damian akizungumza mara baada ya mkuu wa Mkoa wa Dodoma kupokea msaada wa Vitanda na magodoro 40 za hospitali za Mkoa hou ikiwa Exim Bank Tanzania ikiwa kwenye mradi wa kupunguza upungufu wa vitanda na magodoro katika hospitali za hapa nchini.
Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim, Bwana Stanley Kafu akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa benki ya Exim Tanzania mara baada ya kukabidhi magodoro na vitanda 40 katka hospitali za mkoa wa Dodoma. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Binilith Mahenge akisikiliza kwa makini

 HOSPITALI na kliniki nyingi nchini zina tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa. Kama sehemu ya kampeni yake yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii, Benki ya Exim Tanzania imekabidhi vitanda na magodoro 40 kwa Hospitali ya rufaa iliyoko Dodoma.

Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma, mwezi wa Agosti mwaka huu, kwa kuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujali jamii” ambao Benki hiyo itawekeza katika sekta ya afya Tanzania. Mradi huu unalenga kusaidia upungufu wa vitanda katika hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro and vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim, Bwana Stanley Kafu alisema, “ Mwaka huu benki ya Exim imefikia hatua muhimu sana. Tunasheherekea miaka 20 ya uvumbuzi na kujitolea kwa jamii. Kwa miaka mingi benki ya Exim imewekeza kwa kiasi kikubwa katika sekta ya afya, mazingira na elimu nchini. Tunatambua juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya hivyo basi tumejitolea mwaka huu mzima kuwekeza katika hospitali za serikali katika maeneo mbalimbali nchini.” 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr. Bilinith Satano Mahenge alipongeza Exim Bank Tanzania kwa ahadi yake ya kukabiliana na upungufu wa vitanda kwenye ma hospitali ambao unakabiliwa na taifa na kuleta juhudi zake kwa hospitali ya rufaa ya Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...