Gari aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T 928 BLQ ikiwa imeigonga Basi aina ya Scania linalo julikana kwa jina la Safari Njema katika Barabara ya Morogoro eneo la Kibamba kwa Mangi. inadaiwa kwamba Hiace hiyo ilihama njia na kulifata basi lilipokuwa likajiribu kulipita lori na kusababisha watu kadhaa waliokuwepo ndani ya Hiace hiyo kujeruhiwa.
Majeruhi waliokuwa ndani ya Hiace hiyo wakiwa wamelala chini baada ya gari yao kwenda kugonga Basi la Safari njema.
Dereva wa Hiace iliyogonga basi akibebwa kupakiwa kwenye moja ya gari ili kuwahishwa Hospitalai ya Tumbi Kibaha kwa matibabu.
Askari wa usalama Barabarani akiandika Pf 3 kwa Majeruhi wa Hiace iliyogonga Basi la Safari Njema eneo la Kibamba kwa Mangi jijini Dar es Salaam leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...