Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla
(kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya
Ziwa Manyara, Noelia Myonga kuhusu hifadhi hiyo alipoitembelea jana mkoani
Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa
lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla
akigusa maji ya moto ya asili ambayo ni kivutio cha kipekee cha utalii
kilichopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo
jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na
utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. Maji hayo
yanakadiriwa kuwa na nyuzi joto 80 ambapo imeelezwa kuwa baadhi ya watalii
huweza kuchemsha mayai katika maji hayo. Nyuma yake anayeshuhudia ni Mhifadhi
Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla
(kushoto) akionyeshwa maeneo ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara na Mhifadhi
Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga alipoitembelea hifadhi hiyo jana mkoani
Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa
lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini.
Ndege aina mbalimbali wanapatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...