Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani akiwa na kitabu cha wageni kwenye Ofisi ya Serikali ya
Mtaa wa Malindi Estate ambayo ipo kwenye nyumba ya mmoja wa wagombea wa Uchaguzi Mdogo
wa Madiwani Kata ya Mbweni. Picha na NEC.
Hussein Makame-NEC
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imejiridhisha kuwa uamuzi wa
kuvihamisha vituo 21 vya kupigia kura katika Kata ya Mbweni, jimbo
la Kawe katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, umezingatia
Sheria na Kanuni za Uchaguzi.
NEC imetoa msimamo huo, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa
baadhi ya wananchi na vyama vya siasa wakilalamika kuwa Tume ya
uchaguzi imehamisha vituo vinane (8) vya kupigia kura na kuvipeleka
kwenye Kituo cha Polisi, hatua waliyoeleza kuwa ni kuwanyima haki
wapiga kura katika kutimiza haki ya msingi.
Malalamiko mengine yaliyoifikia NEC ni kwamba Tume ilivihamisha
vituo vingine 15 kutoka maeneo ya awali na kuvipeleka maeneo
mengine jambo ambalo baadhi ya vyama havikukubaliana na uamuzi
huo.
Kutokana na malalamiko hayo, jana Jumanne Mkurugenzi wa
Uchaguzi wa NEC, Kailima Ramadhani akiambatana na watendaji
wengine wa Tume, walitembelea maeneo hayo na kujiridhisha kuwa
mabadiliiko ya vituo yaliyofanywa na msimamizi wa uchaguzi
yamekidhi matakwa ya kisheria.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...