Mgeni rasmi, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akifungua semina kuhusu maadili na mapambano dhidi ya rushwa kwa Wanachama wa Chama cha Mtandao wa Wabunge wanaopambana na Rushwa Tanzania (APNAC) iliyofanyika leo katika hoteli ya Morena Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akifuatilia semina kuhusu maadili na mapambano dhidi ya rushwa kwa Wanachama wa Chama cha Mtandao wa Wabunge wanaopambana na Rushwa Tanzania (APNAC) iliyofanyika leo katika hoteli ya Morena Mjini Dodoma. wa pili kulia ni katibu wa Bunge, Mheshimiwa Stephen kagaigai, wa pili kushoto ni katibu wa Chama hicho, Mheshimiwa Daniel Mtuka na kushoto ni kaimu Mwenyekiti wa Chama hicho, Mheshimiwa Cecilia Pareso.

Wanachama wa Chama cha Mtandao wa Wabunge wanaopambana na Rushwa Tanzania (APNAC) wakifuatilia semina kuhusu maadili na Mapambano dhidi ya rushwa iliyofanyika leo katika hoteli ya Morena Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge Mheshimiwa, Job Ndugai (kulia) akipokelewa na Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Mtandao wa Wabunge wanaopambana na Rushwa Tanzania (APNAC), Mheshimiwa Cecilia Pareso (kushoto) kwenda kufungua semina kuhusu maadili na Mapambano dhidi ya rushwa iliyofanyika leo katika hoteli ya Morena Mjini Dodoma.(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...