Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Balozi mpya wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Balozi Wang ke (kulia) alipotembelea leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (katikati) akizungumza na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto), Balozi mpya wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Balozi Wang ke (wa pili kushoto), pamoja na ugeni kutoka ubalozi wa China nchini Tanzania, katika kikao kilichofanyika leo katika Ofisi ya Spika Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Balozi mpya wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Wang ke (wa pili kushoto) katika kikao kilichofanyika leo katika Ofisi ya Spika Mjini Dodoma, katikati ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson na Wageni wengine ni wasaidizi wa Balozi kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania.
Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (kulia) akipokea zawadi toka kwa Balozi mpya wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Wang ke (kushoto) baada ya kikao kilichofanyika leo katika Ofisi ya Spika Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Balozi Wang ke (kulia), Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (kushoto) baada ya kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...