Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekuwa ni Taasisi bora kwa Bara la Afrikakatika kudhibiti dawa na chakula ili watanzania wapate huduma bora.

Ummy ameyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Maabara Hamishika jijini Dar es Salaam, amesema kuwa katika kulinda afya za  wananchi ni kupata dawa zinazostahili ambazo zimedhibitiwa na TFDA.Amesema kuwa matumizi ya dawa zisizo sahihi zinarudisha kasi ya uchumi ambayo inatokana na watu kuingia  gharama za kununua dawa hizo mara kwa mara na tatizo kubaki pale pale.

Ummy amesema kuwa licha ya kudhibiti dawa lakini TFDA isiwe kikwazo cha uwekezaji katika sekta ya viwanda ambapo wawekezaji wanatakiwa kufuata taratibu za nchi zilizowekwa.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maabara hamishika hizo, wakwanza kushoto ni mwakilishi kutoka WHO Dkt. Matthius Kamwa, watatu kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya TFDA Bi. Zainabu na wa mwisho ni Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo Hiiti B. Sillo.
Mh. Ummy Mwalimu akipata maelekezo kuhusu Maabara hamishika hiyo wakati wa uzinduzi wa maabara hamishika mapema leo katika ofisi za Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi wa kwanza kushoto ni mwakilishi kutoka WHO Dkt. Matthius Kamwa.
 Meza kuu ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa maabara hamishika mapema katika ofisi za Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...