Na Karama Kenyunko, Glogu ya Jamii.
Mkurugenzi wa Mashtaka ya jinai (DPP) ameomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwapa siku 14 ili kukamilisha utaratibu wa kupeleka taarifa za kesi ya uhujumu uchumi na kuisababishia serikali hasara ya USD 527,540, Mahakama kuu.
Kesi hiyo inawakabili vigogo wa Kampuni Hodhi ya Mali za Reli (Rahco), Benhardard Tito aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji, Mwanasheria wa Rahco, Emmanuel Massawe na mfanyabiashara ambaye pia ni mwakilishi wa kampuni ya Rothschild (South Africa) Proprietary Limited, Kanji Mwinyijuma.
Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Maghela Ndimbo amewasilisha ombi hilo leo Novemba 2, 2017 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa
Kufuatia maelezo hayo, Hakimu Simba ametoa ahirisho la mwisho na kuwaeleza upande wa mashtaka kuwa ataifuta kesi hiyo kwa kiwango ambacho washtakiwa hao hawatakamatwa tena.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...