Injinia Mratibu wa maswala ya Mazingira Baharini kutoka ZMA Halfani Hamad Hassan kulia akitoa maelezo kuhusiana na zoezi la vitendo la Udhibiti wa Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini katika Mkutano wa kufunga mafunzo hayo uliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
Mkuu wa Kituo cha Huduma za Dharura Norwey Helge Munkas Andersen kushoto akionesha namna ya zoezi zima la mafunzo ya Udhibiti Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini katika Mkutano wa kufunga mafunzo hayo uliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
Mkuu wa Kituo cha Huduma za Dharura Norwey Helge Munkas Andersen akijibu baadhi ya maswala yalioulizwa katika Mkutano wa Ufungaji mafunzo ya Udhibiti Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini uliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhi mjini Unguja.
Naibu Katibu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji, Shomari O,Shomari akitoa hotuba ya ufunguaji wa mafunzo ya Udhibiti Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini yaliochukua muda wa siku Tatu hafla iliofanyika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
Naibu Katibu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Shomari O,Shomari (kulia) akimkabidhi cheti cha Ushiriki wa mafunzo ya Udhibiti Usambaaji wa mafuta yaliomwagika Baharini Injinia Mratibu wa maswala ya Mazingira Baharini kutoka ZMA Halfani Hamad Hassan katika ufungaji wa mafunzo hayo katika Hoteli ya Marumaru Forodhani mjini Unguja.
PICHA NA YUSSUF SIAMI/MAELEZO ZANZIBAR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...